STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 28 Novemba 2015

KILI STARS MWENDO MDUNDO YATINGA ROBO FAINALI SASA KUWAKABILI ETHIOPIA................

Tokeo la picha la CECAFA SENIOUR CHALLEGE ETHIOPIA 2015

TANZANIA Bara imefuzu kwa kishindo Robo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge kufuatia kumaliza mechi za makundi bila kupoteza mchezo.
 
Bara imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na wenyeji Ethiopia katika mchezo wake wa mwisho wa Kundi A leo Uwanja wa Taifa wa Addis Ababa. Dakika 45 za kwanza zilimalizika bila ya timu hizo kufungana na kipindi cha pili, Kilimanjaro Stars ilianza kupata bao kupitia ka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simon Msuva.
 
Msuva alifunga bao hilo la pili kwake katika mashindano ya mwaka huu kwa kichwa dakika ya 51 akimalizia krosi maridadi ya beki wa kushoto, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.
 
Hata hivyo, Wahabeshi walifanikiwa kupata bao la kusawazisha baada ya beki Salum Mbonde kujifunga katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na Mohamed Naser dakika ya 90 na ushei.
 
Stars sasa inamaliza kileleni mwa Kundi A kwa pointi zake saba, ikifuatiwa na Rwanda iliyomaliza na pointi sita, Ethiopia pointi nne, wakati Somalia inaondoka mikono mitupu.
 
Mchezo wa kwanza leo, bao la dakika ya 70 la Frank Kalanda limeipa Uganda ushindi wa 1-0 dhidi ya Burundi.
 
Uganda imemaliza kileleni mwa Kundi B kwa pointi zake sita, ikifuatiwa na Kenya pointi nne ambazo zote zinafuzu moja kwa moja Robo Fainali.  
 
Sasa Tanzania Bara itamenyana tena na Ethiopia katika Robo Fainali Jumatatu, wakati Uganda itacheza na Malawi katika mchezo wa kwanza keshokutwa.
Jumanne Sudan Kusini itacheza tena na Sudan, wakati Rwanda itamenyana na Kenya. 
 
Kikosi cha Tanzania Bara kilikuwa; Aishi Manula, Hassan Kessy, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Salum Mbonde, Kevin Yondan, Himid Mao, Said Ndemla, Jonas Mkude, John Bocco, Elias Maguri na Simon Msuva.
 
Ethiopia; Abel Mamo, Seyoum Tesfaye, Najib Sani, Anteneh Tesfaye, Yared Bayeh, Aschalew Tamene, Panom Gathuoch, Beneyam Tesfaye, Behaylu Girma, Yissack Bereket na Mohamed Naser.
 
 RATIBA ROBO FAINALI KOMBE LA KAGAME 2015
 
Novemba 30, 2015 
Uganda Vs Malawi
Tanzania Bara Vs Ethiopia
Desemba 1, 2015
Sudan Kusini Vs Sudan
Rwanda Vs Kenya

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox