STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 3 Desemba 2015

REAL MADRID HATARINI KUONDOLEWA KWENYE KOMBE LA MFALME BAADA YA KUMPANGA MCHEZAJI ALIYEFUNGIWA

KIUNGO wa Real Madrid, Denis Cheryshev amesisitiza kutopokea taarifa yeyote kutoka klabu yake ya zamani au Shirikisho la Soka la Hispania kumfahamisha alikuwa bado katika adhabu katika mchezo wa Kombe la Mfalme dhidi ya Cadiz uliochezwa jana. 
 
Cheryshev ambaye alifunga bao la kuongoza katika ushindi mabao 3-1, alikuwa na kadi tatu za njano katika klabu yake ya zamani ya Villarreal katika michuano hiyo msimu uliopita ambazo zinamfanya kupata adhabu ya kutocheza mechi moja msimu huu. 
 
Lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye aliichezea Villarreal kwa mkopo msimu uliopita amesisitiza hajapata taarifa yeyote kuhusiana na adhabu hiyo. 
 
Klabu ya Cadiz imethibitisha kuwa wanatarajia kutuma malalamiko yao rasmi kuhusiana na tukio hilo ambalo linaweza kupelekea Madrid kuondolewa katika michuano hiyo. 
 
Klabu ya Osasuna walienguliwa katika michuano ya Kombe la Hispania Septemba mwaka huu baada ya kumtumia mchezaji Unai Garcia ambaye alikuwa katika adhabu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox