STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 10 Desemba 2015

TANZIA KATIKA SOKA,MCHEZAJI AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI...........

 Tokeo la picha la bastola


Mchezaji wa timu ya taifa Honduras Arnold Peralta amepigwa risasi akiwa likizoni mji wake wa kuzaliwa wa La Ceiba.
 Peralta


Aliuawa katika maegesho ya magari katika mji huo, ambao unapatikana katika pwani ya taifa hilo.

Kiungo huyo wa kati wa umri wa miaka 26, ambaye amekuwa akichezea klabu ya Olimpia, katika mji mkuu Tegucigalpa, alichezea klabu ya Rangers ya Scotland hadi Januari.

Visa vya watu kupigwa risasi Honduras huwa juu sana na taifa hilo lina mojawapo ya viwango vya juu zaidi vya mauaji duniani.
 Peralta

Mkurugenzi wa michezo wa shirikisho la soka la Honduras Osman Madrid, alisema mauaji hayo ni ya kusikitisha na kwamba taifa hilo linaomboleza.

Haijabainika nini kilichosababisha mauaji hayo lakini polisi wanasema hakikuwa kisa cha wizi kwani hakuna kitu chochote kilichoibiwa.
Aliwakilisha Honduras katika Michezo ya Olimpiki 2012 jijini London lakini hakuweza kucheza Kombe la Dunia Brazil mwaka 2014 kutokana na jeraha.

Alitarajiwa kuchezea timu ya taifa mechi ya kirafiki dhidi ya Cuba wiki ijayo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox