STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 10 Desemba 2015

RATIBA NZIMA YA LIGI KUU TANZANIA BARA MPAKA DESEMBA 26.............................

  Tokeo la picha la FOOTBALL PITCH
 
RATIBA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA…
Desemba 12, 2915
Kagera Sugar vs Ndanda FC
Stand United vs Mwadui FC
Mbeya City vs Mtibwa Sugar
Azam FC vs Simba SC
Majimaji vs Toto Africans
Mgambo JKT vs Yanga SC
 
Desemba 13, 2015
JKT Ruvu vs Prisons
Coastal Union vs African Sports
Desemba 16, 2015
 
African Sports vs Yanga SC
Desemba 19, 2015
 
Yanga Africans vs Stand United
Mwadui FC vs Ndanda FC
Kagera Sugar vs African Sports
Prisons vs Mtibwa Sugar
Toto Africans vs Simba SC
Majimaji vs Azam FC
 
Desemba 20, 2015
JKT Ruvu vs Coastal Union
Mbeya City vs Mgambo JKT
 
Desemba 23, 2015
Azam FC vs Mtibwa Sugar
 
Desemba 26, 2015
Ndanda FC vs JKT Ruvu
Yanga SC vs Mbeya City
 
 Tokeo la picha la MTIBWA SUGAR FC

LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inarejea kesho baada ya mapumziko ya takriban mwezi mzima kupisha mechi za timu ya taifa na michuano ya Kombe la CECAFA Challenge.
 
Nyasi za viwanja sita zitawaka moto kesho, lakini macho na masikio ya wengi vitaelekezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ambako vigogo Simba SC watakuwa wanamenyana na Azam FC.
 
Azam FC wanahitaji ushindi katika mchezo wa kesho kujiimarisha kileleni na kuzidi kuwaacha mabingwa watetezi, Yanga SC wakati Simba SC inahitaji ushindi ili kurudi kwenye mbio za ubingwa.
 
 Tokeo la picha la SIMBA SC
Na hapo ndipo ulipolalia utamu na msisimko wa mchezo huo, kiasi kwamba hata mashabiki wa Yanga ingawa timu yao itakuwa Uwanja wa Mkwakwani kesho ikimenyana na Mgambo JKT, lakini watakuwa wanasikilizia kinachoendelea Taifa.
 
Na sana Yanga SC wanaitakia ushindi Simba SC au hata sare, ili mahasimu wao hao, Azam FC katika mbio za ubingwa wapunguzwe kasi. 
 
Simba SC imeimarisha kikosi chake katika dirisha dogo kwa kumrejesha mshambuliaji wake Mkenya, Paul Kiongera aliyekuwa anacheza kwa mkopo KCB ya kwao.
 
 Tokeo la picha la AZAM FC
Aidha, Wekundu hao wa Msimbazi pia wamesajili chipukizi wawili, beki wa kati Novat Makunga kutoka African Sports ya Tanga na mshambuliaji Hajji Ugando kutoka Mtibwa Sugar B, ingawa haijulikani kama watakamilishiwa utaratibu wa kupata leseni kabla ya mechi za kesho.
 
Azam FC yenyewe imemsajili kipa mkongwe, Ivo Mapunda aliyewahi kudakia Yanga SC, Tukuyu Stars, Prisons, Moro United, African Loyon, Simba za Tanzania pia na St George ya Ethiopia na Gor Mahia ya Kenya.
 
Mabingwa watetezi, Yanga SC wao kesho watakuwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kumenyana na timu ngumu, MGambo JKT ya Kabuku, Tanga.  
 Tokeo la picha la YANGA FC
 
Mechi nyingine za ligi hiyo kesho; Kagera Sugar wataikaribisha Ndanda FC Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Stand United wakiongozwa na kinara wa mabao Ligi Kuu, Elias Maguri wataikaribisha Mwadui FC, Mbeya City wataikaribisha Mtibwa Sugar, Majimaji wataikaribisha Toto Africans, wakati Jumapili JKT Ruvu watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Karume na Coastal Union watamenyana na mahasimu wao, African Sports.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox