Ligi kuu ya nchini Ufaransa ambayo imeanzishwa 1923 ni miongoni mwa ligi kubwa tano barani Ulaya kwa hivi sasa huku ikijumuisha wachezaji kutoka mabara mbalimbali ikiwemo barani Afrika.
Wikendi hii tulishuhudia tuzo mbalimbali zikitolewa kwa waliofanya vizuri katika msimu wa 2015-2016 msimu ambao Paris Saint German wamefanikiwa kutetea ubingwa wao.
Tuzo hizo ni mchezaji bora wa msimu ambapo washindani walikuwa ni Zlatan Ibrahimovic, Angel Di Maria wote wa Psg , Hatem Ben Arfa wa Nice na kiungo wa Marseille Lassana Diarra na mwisho wa siku mshambuliaji wa Psg Zlatan Ibrahimovic, mwenye magoli 35 msimu huu kufanikiwa kushinda tuzo hiyo kwa mara ya tatu mfululizo.
Kocha wa Psg, Mfaransa Laurent Blanc amefanikiwa kushinda tuzo ya kocha bora wa msimu ikiwa ni mara ya pili mfululizo huku kinda mwenye miaka 18 wa klabu ya Rennes mshambuliaji Ousmane Dembele akichukua tuzo ya chipukizi bora wa msimu.
Ligue 1 Goalkeeper of the Year - Steve Mandanda (Marseille)
Golikipa bora ni Steve Mandanda wa Marseille akimshinda kipa wa Lille ambae alipewa chapuo huenda angeshinda mnigeria Vincent Enyeama wakati goli bora la msimu ambalo limechaguliwa lilifungwa na Pierrick Capelle wa Angers SCO katika mchezo dhidi ya EA Guingamp.
Ligue 1 Young Player of the Year – Ousmane Dembélé (Rennes)
Ligue 1 Coach of the Year – Laurent Blanc (Paris Saint-Germain)
KIKOSI BORA CHA MSIMU 2015-2016-
Steve Mandanda (Marseille); Maxwell (PSG), David Luiz (PSG), Thiago Silva (PSG), Serge Aurier (PSG); Blaise Matuidi (PSG), Lassana Diarra (Marseille), Marco Verratti (PSG); Hatem Ben Arfa (Nice), Zlatan Ibrahimovic (PSG), Angel di Maria (PSG)
-->
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni