KIPA wa kikosi cha timu
ya taifa ya wanawake ya Cameroon, Jeanine Christelle Djomnang amefariki
dunia baada ya kuanguka wakati akifanya mazoezi ya kupasha
misuli.
Shirikisho la Soka la nchini hiyo-Fecafoot, limedai kuwa
Djomnang mwenye umri wa miaka 26, aliugua kabla ya mchezo wa timu yake
ya Femina Stars Ebolowa huko kusini mwa Cameroon jana na alifariki
wakati akikimbizwa hospitali.
Taarifa za awali kutoka Fecafoot zinadai
kuwa mchezaji huyo alifariki kwa shambulio la moyo lakini kwasasa bado
wanasubiri taarifa ya kitabibu.
Taarifa hizo zinakuja siku chache baada
ya mchezaji mwingine wa nchi hiyo Patrick Ekeng kufariki dunia baada ya
kuanguka katika mchezo wa Ligi Kuu huko Romania.
Inadaiw kuwa Djomnang
alikuwa akilalamika maumivu ya kifua wakati wakijiandaa na mchezo huo wa
ligi kabla ya kuanguka na kukimbizwa hospitali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni