Klabu ya Manchester United kwa muda mrefu imekuwa ikihusishwa na taarifa za kumuwania kiungo mshambuliaji wa Benfica Renato Sanches ambae amekuwa na kiwango bora kabisa katika klabu hiyo ya nchini Ureno sehemu ambayo ndipo alipokulia kisoka.
Karl-Heinz
Rummenigge (left)Sanches (right)
Taarifa za kujiunga kwake Manchester United zilizidi kushamiri mara baada ya kocha Jose Mourinho kuhusishwa kuchukua nafasi ya Louis Van Gaal kama kocha mkuu wa klabu hiyo msimu ujao.
Hayo yalikuja kutokana na wakala wa Mourinho ,Jorge Mendes kuwa pia ni wakala wa Renato Sanches.
Taarifa zilizotoka ni kwamba Renato Sanches amejiunga rasmi na mabingwa wa Bundasliga, Bayern Munich kwa mkataba wa miaka mitano akinunuliwa kutoka Benfica kwa £28m.
Kocha mpya wa Bayern Munich Carlo Ancelotti
Wakati huo;
Habari kutoka Ujerumani zinasema
Hummels,27 amesaini mkataba wa miaka mitano wa kuitumikia Bayern Munich.Mkataba
huo utafikia ukomo Juni 30,2021.
Hii ni kama Hummels amerudi nyumbani
kwani safari yake ya kucheza soka ilianzia katika shule ya soka ya Bayern
Munich kabla ya mwaka 2008 kutua Borussia Dortmund kwa uhamisha wa mkopo ambao
baadae ulifanywa kuwa wa kudumu.
Hummels anakuwa mchezaji wa tatu
kuhamia Bayern Munich katika kipindi kisichozidi miaka mitatu.Wa kwanza alikuwa
Mario Gotze kisha akafuatiwa na Robert Lewandowski.
Hummels atajiunga na Bayern Munich
Juni 1 baada ya kumalizika kwa mchezo wa fainali wa kombe la DFB-Pokal
utakaochezwa Mei 21 kati ya Borussia Dortmund na Bayern Munich.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni