Hassan Kessy ametia saini juzi mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili kuanzia mwezi ujao (June, 2016).
Awali Kessy alikuwa akiitumikia klabu ya Simba kabla ya
kufungiwa mechi tano na wekundu hao wa Msimbazi kwa madai ya kuigharimu timu kutokana na kitendo cha kuoneshwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Toto Africans mchezo uliomalizika kwa Simba kupoteza kwa bao 1-0.
Licha ya Simba kumfungia Kessy, tayari beki huyo mwenye uwezo mkubwa wa kukaba na kupandisha mashambulizi mkataba wake na Simba unamalizika mwisho wa msimu huu na klabu hiyo haikuonesha nia ya kuhitaji huduma ya nyota huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni