STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 10 Oktoba 2016

KWA MARA YA KWANZA KADI YA KIJANI IMETOLEWA NA KUANDIKA HISTORIA MPYA KWENYE SOKA


Wiki hii historia mpya imewekwa nchini Italy baada ya mshambuliaji wa Vicenza inayoshiriki Ligi ya Serie B, Cristian Galano kuzawadiwa kadi ya kijana kwa kucheza mchezo wa kiungwana (fair play).

Maafisa wa soka nchini Italy mwanzoni mwa msimu huu walitangaza matumizi ya kadi hiyo na kusema mchezaji atayekuwa na kadi nyingi zaidi za kijana atapewa zawadi mwishoni mwa msimu.

Kadi hiyo ilitolewa baada ya Galano kukiri kwa mwamuzi kuwa, hakukuwa na beki yeyote wa Virtus Entella aliyegusa mpira ambao mwamuzi Marco Mainardi aliamuru kupigwa kona.

Rais wa Serie B Andrea Abodi amekiri kwamba kadi hiyo ipo kama alama tu, lakini yenye mantiki ya kuifanya ligi hiyo kuwa na mtazamo chanya kufuatia kukabiliwa na tuhuma mbalimbali za upangaji matokeo.

"Ni kadi ambayo ipo kama alama tu," amesema "Ni kitu rahisi tu. jambo muhimu hapa ni kujua tu kwamba mtu hupewapindi anapofanya jambo la kiweledi zaidi.

“Sisi tunaamini kwamba mchezo wa soka unahitaji ujumbe weye kuijenga jamii yenye mtazamo chanya,” Ofisa Habari wa Serie B aliongeza.


“Kumbuka mchezo huu wakati mwingine unaweza kusababisha hasira kwa watu mpaka wakatoka uwanjani.”




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox