STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 21 Oktoba 2016

MANJI AFUNGUKA KUELEKEA MKUTANOWA TAREHE 23 MWEZI HUU........

Tokeo la picha la yusuphu manji
 
WANACHAMA wa klabu ya Yanga wametakiwa kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano mkuu wa dharura utakaofanyika Oktoba 23 Makao makuu ya klabu Jangwani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili masuala mbali mbali likiwemo suala la ukodishwaji.



Tokeo la picha la yusuphu manji 

Mwenyekiti wa Klabu hiyo Yusuph Manji amewaambia waandishi wa Habari kuwa mkutano huo utakuwa wa wazi na kila mwanachama atapewa nafasi ya kutoa maoni yake juu ya suala zima la uendeshwaji kwa ajili ya maendeleo ya Yanga.

Manji alisema badala ya wanachama kukimbilia kwenye vyombo vya Habari kuongea kuhusu masuala ya klabu wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano huo ili kuchangia kwa manufaa ya Yanga.

"Mkutano utakuwa huru na wa haki kila mwanachama ambaye amelipia kadi yake atapewa nafasi ya kutoa duku duku lake kabla ya makubaliano kufikiwa," alisema Manji.

Manji alisema baada ya makubaliano hayo kufanyika Uwanja wa mazoezi utaanza kujengwa ndani ya siku 90 katika eneo la Gezaulole lililopo Kigamboni kwa mujibu wa mkataba uliosainiwa na kampuni ya Yanga.

Aidha Manji alisema kuhusu suala la kusainiwa kwa mkataba na bodi ya wadhamini dhidi ya kampuni ya Yanga Yetu kila kitu kitajadiliwa kwenye mkutano huo ambapo wanachama wametakiwa kuwahi mapema huku ulinzi ukiwa ni uhakika.



Wakati huo Yusuph Manji amemtaka Katibu wa Baraza la Wazee Mzee Ibrahim Akilimali kuhudhuria kwenye mkutano mkuu wa dharura utakaofanyika Jumapili Oktoba 23 kama amelipia kadi yake ya uanachama kwa mujibu wa katiba ya Yanga.

Mzee Akilimali pamoja na wazee wenzake wa Baraza hilo walijitokeza hadharani mapema wiki hii kuupinga mkutano huo kwa madai kuwa umekiuka katiba ya Yanga na pia suala zima la ukodishwaji wa nembo ya timu hiyo ni batili kutokana na bodi ya udhamini iliyosaini mkataba na kampuni ya Yanga Yetu kuwa haipo kisheria kwavile ni ya mpito na haikusajiliwa RITA.

Manji alisema mbele ya Waandishi wa Habari kuwa wanachama wote wa klabu ya Yanga akiwemo Mzee Akilimali wanapaswa kuhudhuria kwenye mkutano huo utakaofanyika klabuni hapo kuanzia saa 3 asubuhi lakini lazima wawe wamelipia kadi zao za uanachama.

"Watakaoruhusiwa kushiriki mkutano huo ni wale tu waliolipia kadi zao za uanachama kwahiyo kama Mzee Akilimali amelipia basi aje mkutanoni atapewa nafasi ya kutoa maoni yake kuhusu mustakabali wa timu yetu kwa sababu tunahitaji mshikamano ndani ya Yanga," alisema Manji.

Kumekuwa na taarifa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa Katibu huyo hajalipia kadi yake kwa ziada ya miezi sita kitu ambacho ni kinyume na katiba ya klabu hiyo ambayo itamfanya kushindwa kushiriki kwenye mkutano huo.

Mzee Akilimali mwenyewe alisema mbele ya Waandishi wa Habari mapema wiki hii kuwa hatahudhuria mkutano huo kwavile umekiuka katiba ya klabu hiyo.


 AJENDA ZA MKUTANO WA JUMAPILI KAUNDA
 
1. SALA NA UTAMBULISHO WA WAGENI WAALIKWA:
 
1.1. Sala ya Wakristo ya Kubariki Kikao.

 
1.2. Sala ya Waislamu ya Kubariki Kikao.

 
1.3. Utambulisho wa wageni waalikwa waliohudhuria, pia wenye udhuru – Waziri wa Michezo na Sanaa; Mwenyekiti wa Baraza la Michezo (BMT), Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Dar-Es-Salaam (DRFA) na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
2. Kufungua kikao.

 
3. Kupitia dondoo za kikao kilichopita cha mkutano wa wanachama na kuidhinisha.

 
4. Kuthibitisha wajumbe wa bodi ya wadhamini na kumpumzisha mjumbe mmoja na kuongeza mjumbe mwingine kwenye baraza la wadhamini. mwenyekiti kuomba ridhaa ya kumteua mjumbe mmoja bila ya kuitisha mkutano mkuu kupunguza gharama kwaklabu. 

 
5. Kupitia na kujadill muhtasari ya makubaliano ya bodi ya wadhamini kulingana na maagizo ya wanachamakukodisha timu ya yanga na nembo ya yanga kwa kipindi cha miaka kumi/ na kupata maamuzi kupitia kura za wanachama. 

 
6. KujadiliMmweyekiti abaki kama mwenyekiti au kulingana na maslahi yake kwenye kampuni, kama italeta mgongano katika kampuni yake inayokodisha timu ya yanga na nembo ya yanga kwa kipindi cha miaka kumi  ili kupata maamuzi kupitia kura za wanachama.

 
7. Kurudia kupitia marekebisho ya katiba iliyoagizwa na wanachama kupitia vikao vyao mbalimbali na baadhi kukataliwa natff, baadhi hazijasajiliwa kazi na bmt na baadhi rita wamezikalia bila kuzifanyia kazi kwa sababu zisizojulikana. kupata msimamo wa wanachama kwa kuzingatia katiba ya yanga inayosema mikutano ya wanachama ndio yenye mamlaka ya mwisho ilimradi tu maamuzi hayo yaangukie ndani ya sheria za nchi.  na si sahihi vyombo hivyo kuingiliaa maamuzi halali ya wanachama.

 
8. Kupitia utendaji wa kamati ya mashindano, ratiba ya ligi kuu bara, adhabu ya yanga kutoka wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo ambayo ilisababishwa na fujo za mashabiki wa simba.   

 
9. Kupata maamuzi juu ya wanachama ambao hawafiki katika mikutano badala yake wanakuwa wasemaji wa yanga bila kuwa na mamlaka hayo na kuleta uchonganishi wa wazi ndani ya klabu, kupotsoha jamii nakuchafua majina ya viongozi wa klabu.

 
10. Tarehe ya uchaguzi mdogo kujazia nafasi zilizo wazi na kupata mwongozo wakutumia katiba ipi kati ya 2010 au 2014.pamojana masahihisho baada ya 2014, au bila ya masahihisho ya 2014 yaliyoamuliwa na wanachama.

 
11. Hotuba ya Mwenyekiti –maoni na msimamo wake juu ya maazimio ya wanachamakwenye kikao; kusema anayoyajua ya siri kuhusu yanga na adui wa Yanga na kufafanua wanaoleta vurugu Yanga, baadhi ni mamluki wa wafanyabiashara wenzake walioshindwa kumshinda kwa njia halali na sasa wanaitumia yanga kama sehemu pekee iliyobaki kumuumiza kupitia mbinu zinazotumika hasa kwa kuleta vurugu ndani ya yanga ili kumchafua yeye binafsi, kufanya kwao hivyo ni kushusha hadhi ya klabu na maoni yake kwa maslahi ya yanga, kipi kifanyike.

 
12. Mengeniyo.
13. Sala.
13.1. Sala ya waislamu ya kubariki maamuzi ya mkutano. 
13.2. Sala ya wakristo kubariki maamuzi ya mkutano.
14. Kufunga mkutano.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox