STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 19 Oktoba 2016

TIZAMA MAKUNDI YA AFCON KULE GABON 2017 PAMOJA NA REKODI ZA MESSI USIKU WA UEFA JANA..........


  In contrast, City boss Pep Guardiola shows his frustration at seeing his side concede on 17 minutes
Baada ya Uganda kupangwa Kundi D sambamba na timu za Misri, Ghana, pamoja na Mali kwenye micuano ya AFCON 2017, kocha wa Uganda Cranes Micho Sredojević ametoa wito kwa serikali kuhakikisha timu inapata support ya kutosha kwa ajili ya maandalizi ya mapema.
Licha ya timu yake kupangwa kwenye Kundi gumu, Micho hana budi bali ni kupambana na changamoto iliopo mbele yake.
“Hakuna namna ya kukwepa, unaweza ukasema pengine ndiyo mwisho wetu, ni sawa na Kundi tulilopo kwenye Kombe la Dunia lakini safari hii ni fainali za AFCON dhidi ya Ghana na Misri. Ni kundi gumu lenye ushindani,” alisema Micho mara baada ya draw ya upangaji makundi kukamilika.
Ghana walipoteza kwenye mchezo wa fainali katika michuano iliyopita ya FCON iliyofanyika Equatorial Guinea 2015 dhidi ya Ivory Coast. Misri ni nchi yenye uchu ikiwa imeyakosa mashindano hayo kwa miaka misimu mitatu iliyopita, lakini wakiwa ni mabingwa mara tatu mfululizo waliopta, Mali ndani ya fainali tatu za AFCON wameshika nafasi ya tatu mara mbili, ni kundi gumu.
Ghana na Uganda zilitoka suluhu kwenye mchezo wa ufunguzi wa Kundi E kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 na wanatarajia kucheza mara mbili dhidi ya Misri baada ya michuano ya AFCON kumalizika.
“Ukiangalia kila kitu, utaona tunatakiwa kuanza maandalizi sasa kwa upendo na support kutoka waganda wote, wachezaji na wote wenye wajibu wa kuiandaa timu yetu kuwa timu yenye ushindani, hapa nafikiria maandalizi pamoja na mechi za kirafiki ambapo tutakuwa makini na kila taarifa. Naamini katika soka hakuna kinachoshindikana bali kila kitu kinawezekana.”
“Ninaiamini timu na wachezaji tulionao, naamini katika kile tunachokifanya, ninaamini serikali ya Uganda itatusaidia kuhakikisha tunaliwakisha taifa katika njia bora.”
“Hatua tuliyofikia ni nusu ya safari, ili safari yetu ikamilike tunahitaji kuanza maandalizi sasa, tunastahili kuwa hapa lakini tunahitaji kuonesha hilo kwa vitendo tukiwa uwanjani na si kwa kuongea.”
Uganda wataanza kampeni yao kwa mchezo wao wa ufunguzi January 17 dhidi ya The Black Stars, kisha watashuka tena uwanjani kukabiliana na mapharao wa Msri January 21 kabla ya kuhitimisha hatua ya makundi dhidi ya Mali January 25.
                                        Makundi;
caf                    





























                          BARANI ULAYA;

         MATOKEO YA MECHI ZOTE ZA UEFA JANA HAYA HAPA




 REKODI YA MESSI;

 

Lionel Messi amefunga hat-trick wakati Barcelona ikiaangamiza Manchester City kwenye mchezo wa Champions League wakati Pep Guardiola akirejea kwenye klabu yake ya zamani.

City walipambana kipindi cha kwanza lakini walifanya makosa mengi ya wazi dhidi ya kikosi cha Barcelona ambacho ndani yake kilikuwa na Messi aliye rejea kutoka majeruhi.

Fernandinho alianguka ndani ya box na kumpa nafasi Messi kupachika bao la pili kabla ya Kelvin de Bruyne kupoteza mpira na kumruhusu Iniesta kumtengenezea muargentina huyo kufunga bao la pili.

 3986d7ad00000578-3852820-image-a-61_1476907442689

Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa wageni ambapo golikipa wao Claudio Bravo alizawadiwa kadi nyekundu kwa kudaka mpira akiwa nje ya box kisha dakika moja baadaye Messi akapachika bao jingine.

 3986d1d300000578-3852820-image-a-60_1476907202301

Barcelona pia walibaki 10 uwanjani kwa dakika 15 za mwisho baada ya Jeremy Mathieu ambaye aliingia kuchukua nafasi ya Gerrard Pique kuoneshwa kadi ya pili ya njano kwa kumfanyia madhambi Raheem Sterling.


Willy Caballero aliokoa mchomo wa Neymar lakini nyota huyo wa Brazil akafunga goli dakika moja baadaye kukamilisha ushindi wa magoli 4-0 wa miamba hiyo ya La Liga.

Ushindi huo uaifanya Barcelona kuendeleza ushindi kwa 100% katika Kundi C na kuendelea kuongoza kwa tofauti ya pointi tano na Manchester City.

Hiki kilikuwa ni kipigo kingine kwa Guardiola akirejea Nou Camp. 

Akiwa kocha wa Barcelona, aliisaidia timu hiyo kutwaa jumla ya mataji 14 lakini sasa amepoteza mara mbili dhidi ya klabu hiyo ya Hispania. Alichezea kichapo cha magoli 3-0 kwenye mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya UEFA Champions Legue akiwa kocha wa Bayern Munich.
  • Lionel Messi amefunga magoli 15 katika mechi 13 za Champions League dhidi ya timu za England.
  • Manchester City wamechezea kipigo kikubwa zaidi kwenye michuano ya Champions League, kwa mara ya kwanza wamefungwa magoli manne.
  • Goli la kwanza la kwenye mchezo huo lilikuwa ni goli la 100 kwa safu ya MSN kwenye mashindano yote kwa mwaka 2016.
  • Messi kwa sasa anaongoza orodha ya wafungaji katika viwanja vya nyumbani kwenye michuano ya Ulaya akiwa mefunga magoli 50.
  • Pep Guardiola ameruhusu magoli 9 kwenye mechi tatu za Champions League dhidi ya Barcelona tangu alivyoondoka kwa miamba hiyo ya Catalan.
  • Barcelona wamekosa mikwaju 11 ya penati kati ya 27 ambayo wamepata katika michuano yote tangu kuanza kwa msimu wa 2015-16.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox