STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 19 Oktoba 2016

YANGA YAICHAPA TOTO, CHIRWA GARI LIMEWAKA ATUPIA TENA



MSHAMBULIAJI wa Obrey Chirwa ameanza kuwajibu waliokuwa wakimbeza kuwa ni 'galasa' baada ya leo kufunga tena kwenye ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Toto African mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Tokeo la picha la CHIRWA YANGA Chirwa alikuwa katika wakati mgumu baada ya kuchelewa kufunga tangu aliposajiliwa toka FC Platinum ya Zimbabwe kwa dau la sh 200 milioni huku wengi wakisema mshambuliaji huyo hakustahili kununuliwa kwa pesa hiyo kulinganisha na ufanisi wake uwanjani. Chirwa alifunga goli lake la kwanza kwenye ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mzimbabwe huyo aliipatia ya Yanga bao la kwanza dakika ya 29 kwa kichwa cha mkizi akimalizia mpira wa krosi uliopigwa na Simon Msuva pembeni kidogo ya eneo la hatari.


Msuva aliifungia Yanga bao la pili kwa mkwaju wa penalti dakika ya 55 baada ya Deus Kaseke kuangushwa na beki wa Toto kwenye eneo la hatari.


Yanga imepanda hadi nafasi ya tatu  baada ya kufikisha alama 18 katika michezo tisa iliyoshuka dimbani pointi tano nyuma ya vinara Simba wanaongoza.


Matokeo mengine ya mechi za Leo

African Lyon 0-2 Majimaji
Ruvu Shooting 1-1 Mwadui FC
Ndanda FC 1-1 Mbeya City
Tanzania Prisons 2-1 Stand United
.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox