DAKTARI wa klabu ya Bayern Munich, Hans-Wilhelm Muller-Wolhfahrt amejiuzulu baada ya kufanya kazi hiyo kwa miaka 38, akidai kuwa kitengo cha afya kinapaswa kulaumiwa kutokana na kipigo walichopata kutoka kwa FC Porto katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Bayern iliwakosa nyota wake kadhaa muhimu katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ambao walichapwa mabao 3-1. Muller-Wohlfahrt mwenye umri wa miaka 72 amesema kutokana na sababu zisizoelezeka ni kitengo cha afya ndio kinapaswa kulaumiwa kwa matokeo hayo. Daktari huyo mkongwe amesema uhahusiano baina ya kitengo hicho na wachezaji umekuwa na mpasuko. Mawinga Franck Riberyn na Arjen Robben, kiungo Bastian Schweinsteiger na beki David Alaba wote walikosa mchezo huo wa Jumanne kwasababu ya majeruhi. Muller-Wohlfahrt ambaye pia amekuwa akifanya kazi kama daktari wa timu ya taifa ya Ujerumani amekuwa akiwatibu wanamichezo maarufu akiwemo bingwa mara sita wa michuano ya olimpiki Usain Bolt kutoka Jamaica.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 17 Aprili 2015
DAKTARI WA BAYERN AJIUZULU KUFUATIA KIPIGO.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni