Timu ya Etoile du Sahel tayari imeshawasili jijini Dar es Salaam ikitokea Tunisia kwa ajili ya mechi ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya wenyeji wao Yanga SC mchezo utakaopigwa kesho kwenye uwanja wa Taifa.
Etoile imewasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere alfajiri ya leo wakiwa na msafara wenye jumla ya watu 56 kati yao wachezaji ni 19, benchi la ufundi likiwa na watu 13, waandishi wa habari 12 na wengine 10.
Msafara huo umepokelewa na afisa ahabari wa Yanga SC Jerry Muro ambaye aliwasindikiza moja kwa moja mpaka kwenye hoteli waliyofikia ambayo ni Ledger Plaza na baadae watafanya mazoezi yao kwenye uwanja wa Taifa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni