STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 12 Julai 2014

RAGE AIKABIDHI RASMI SIMBA SC KWA AVEVA, LAKINI


Kutoka kulia walioketi, Alhaj Rage, Aveva na Ezekiel Kamwaga Katibu wa klabu, wakati nyuma waliosimama kutoka kulia ni Iddi Kajuna, Said Tuliy na Jasmin Badour, wote Wajumbe wa Kamati ya Utendaji wakati wa makabidhiano jana Msimbazi

ALIYEKUWA mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage jana alikabidhi ofisi kwa Rais mpya wa klabu hiyo, Evans Aveva lakini alishindwa kuweka wazi fedha ambazo anaziacha kwenye akaunti ya klabu hiyo.
Gazeti la Nipashe la leo limeandika kwamba, Rage alisema kuwa masuala ya pesa yanahitaji mambo mengi ya kiufundi hivyo atatangaza baadae masuala yote ya pesa.
"Nina imani kubwa na uongozi huu, ninakabidhi kila kitu kwa uongozi mpya lakini suala la akaunti na pesa zilizopo ni suala ambalo nitakaa na uongozi na kuwakabidhi baada ya kukamilisha baadhi ya mambo," alisema Rage.
Rage jana alikabidhi nyaraka mbalimbali kwa uongozi mpya ikiwemo mikataba ya wachezaji na klabu hiyo pamoja na mikataba ya wafanyakazi wengine.
Pia alikabidhi jengo la klabu hiyo na mikataba ya wapangaji pamoja na nyaraka za uwanja wao wa Bunju. pia alikabidhi katiba ya klabu hiyo pamoja na katiba ya Shirikisho la soka nchini (TFF).
Rage alikabidhi vitu hivyo huku akitaka klabu hiyo kuwa na umoja utakaowasaidia kufanya vizuri kwenye mashindano ya ndani pamoja na yale ya kimataifa.
"Nakuomba Rais Aveva, kuimarisha umoja wa klabu pamoja na kuvunja makundi yote, ni vizuri ukakaa pamoja na wanachama waliofungua kesi mahakamani ili kupata suluhu," alisema Rage
Kwa upande wake, Aveva alimshukuru Rage na kusema kuwa ni kiongozi aliyeonyesha moyo wa upendo na kuwasaidia wakiwa kama viongozi wapya wa klabu hiyo.
Alisema kuwa uongozi wa rage ulifanya kazi kubwa na ulikuwa na malengo ya kuhakikisha timu inakuwa katika nafasi nzuri huku wakiwa na mipango mizuri.
Alisema kuwa uongozi wake utaendeleza mambo yote mazuri ambayo uongozi wa rage uliyafanya ili kuhakikisha timu inakuwa katika nafasi nzuri nje na ndani ya uwanja.

MTOTO WA MIAKA SITA AFICHWA CHINI YA UVUNGU WA KITANDA MOROGORO.

  Baada ya kufichuliwa kutoka alipofichwa, mtoto huyo alionekana kuwa dhaifu kiafya kutokana na kukosa lishe pamoja na mazingira aliyokuwa akiishi kutoridhisha, jambo ambalo ni kosa kisheria, pia ukiukwaji wa haki za watoto.

Na Hamida Shariff, Morogoro.   
  Wakati jamii ikiwa bado haijasahau mateso aliyoyapata mtoto Nasra Mvungi na kusababisha  kifo chake, tukio lingine la aina hiyo limetokea katika Kijiji cha Matongola, Tarafa ya Magole Wilaya ya Kilosa, baada ya kubainika mtoto wa miaka sita akiwa amefichwa uvunguni mwa kitanda na kufanyiwa vitendo vya kikatili na mama yake mzazi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonald Paulo alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa taarifa za mateso ya mtoto huyo zilifikishwa Kituo cha Polisi wilayani Kilosa za saa za mchana jana, baada ya uongozi wa  kijiji na kata kutoa taarifa na tayari mwanamke huyo amekamatwa kwa ajili ya mahojiano zaidi.
Mama aliyefanya ukatili huo anafahamika kwa jina la Sala Mazengo ambaye alimficha ndani mtoto wake aliyefahamika kwa jina la Devota Malole na kumfanyia vitendo vya kikatili ikiwa pamoja na kutompa chakula, wala kumfanyia usafi.
Baada ya kufichuliwa kutoka alipofichwa, mtoto huyo alionekana kuwa dhaifu kiafya kutokana na kukosa lishe pamoja na mazingira aliyokuwa akiishi kutoridhisha, jambo ambalo ni kosa kisheria, pia ukiukwaji wa haki za watoto.
Inadaiwa kuwa tangu mwka 2009 Sala amekuwa akimficha mtoto wake huyo ambaye sasa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa ajili ya kupatiwa vipimo na matibabu.
Hata hivyo, mwanamke huyo alipoulizwa alidai kuwa afya ya mtoto wake ilikuwa mbaya tangu alipozaliwa kutokana na magonjwa ya mara kwa mara, pia hali ngumu ya maisha ilichangia kudhoofisha afya ya mtoto huyo.
Alidai kuwa ana watoto sita, pia alikiri kumlaza chini mtoto huyo kutokana na kuwa na kitanda kimoja, ambacho hakiwatoshi watoto hao.
Aliongeza kuwa hata chakula amekuwa akikipata kwa shida kutokana na kushindwa kufanya kazi kwa kuwa ana mtoto mwingine mdogo.
Kamanda Paulo alisema kuwa  mwili wa mtoto huyo umedhoofu kutokana na kufichwa ndani kwa muda mrefu na bado mwanamke huyo hajaeleza sababu za kufanya vitendo vya ukatili dhidi ya mtoto huyo.
“Siwezi kutoa taarifa ya kidaktari, lakini kutokana na afya ya mtoto yule na mazingira tuliyomkuta ni dhahiri alikuwa akipata mateso na kufanyiwa vitendo vya ukatili. Hata hivyo, uchunguzi zaidi tunaufanya na kwamba taratibu za kumfikisha mtuhumiwa huyo Kituo Kikuu cha Polisi mkoani hapa zinaendelea,” alisema Kamanda Paulo.
Alisema kuwa mpaka sasa bado haijafahamika kama mtoto Davota ni mlemavu au la na kwamba taarifa za afya ya mtoto huyo zitatolewa baada ya madaktari kumfanyia uchunguzi wa kina
- See more at: http://ubalozini.blogspot.com/2014/07/mtoto-wa-miaka-sita-afichwa-chini-ya.html#sthash.dTmMOY6p.dpuf

MTOTO WA MIAKA SITA AFICHWA CHINI YA UVUNGU WA KITANDA MOROGORO.

  Baada ya kufichuliwa kutoka alipofichwa, mtoto huyo alionekana kuwa dhaifu kiafya kutokana na kukosa lishe pamoja na mazingira aliyokuwa akiishi kutoridhisha, jambo ambalo ni kosa kisheria, pia ukiukwaji wa haki za watoto.

Na Hamida Shariff, Morogoro.   
  Wakati jamii ikiwa bado haijasahau mateso aliyoyapata mtoto Nasra Mvungi na kusababisha  kifo chake, tukio lingine la aina hiyo limetokea katika Kijiji cha Matongola, Tarafa ya Magole Wilaya ya Kilosa, baada ya kubainika mtoto wa miaka sita akiwa amefichwa uvunguni mwa kitanda na kufanyiwa vitendo vya kikatili na mama yake mzazi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonald Paulo alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa taarifa za mateso ya mtoto huyo zilifikishwa Kituo cha Polisi wilayani Kilosa za saa za mchana jana, baada ya uongozi wa  kijiji na kata kutoa taarifa na tayari mwanamke huyo amekamatwa kwa ajili ya mahojiano zaidi.
Mama aliyefanya ukatili huo anafahamika kwa jina la Sala Mazengo ambaye alimficha ndani mtoto wake aliyefahamika kwa jina la Devota Malole na kumfanyia vitendo vya kikatili ikiwa pamoja na kutompa chakula, wala kumfanyia usafi.
Baada ya kufichuliwa kutoka alipofichwa, mtoto huyo alionekana kuwa dhaifu kiafya kutokana na kukosa lishe pamoja na mazingira aliyokuwa akiishi kutoridhisha, jambo ambalo ni kosa kisheria, pia ukiukwaji wa haki za watoto.
Inadaiwa kuwa tangu mwka 2009 Sala amekuwa akimficha mtoto wake huyo ambaye sasa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa ajili ya kupatiwa vipimo na matibabu.
Hata hivyo, mwanamke huyo alipoulizwa alidai kuwa afya ya mtoto wake ilikuwa mbaya tangu alipozaliwa kutokana na magonjwa ya mara kwa mara, pia hali ngumu ya maisha ilichangia kudhoofisha afya ya mtoto huyo.
Alidai kuwa ana watoto sita, pia alikiri kumlaza chini mtoto huyo kutokana na kuwa na kitanda kimoja, ambacho hakiwatoshi watoto hao.
Aliongeza kuwa hata chakula amekuwa akikipata kwa shida kutokana na kushindwa kufanya kazi kwa kuwa ana mtoto mwingine mdogo.
Kamanda Paulo alisema kuwa  mwili wa mtoto huyo umedhoofu kutokana na kufichwa ndani kwa muda mrefu na bado mwanamke huyo hajaeleza sababu za kufanya vitendo vya ukatili dhidi ya mtoto huyo.
“Siwezi kutoa taarifa ya kidaktari, lakini kutokana na afya ya mtoto yule na mazingira tuliyomkuta ni dhahiri alikuwa akipata mateso na kufanyiwa vitendo vya ukatili. Hata hivyo, uchunguzi zaidi tunaufanya na kwamba taratibu za kumfikisha mtuhumiwa huyo Kituo Kikuu cha Polisi mkoani hapa zinaendelea,” alisema Kamanda Paulo.
Alisema kuwa mpaka sasa bado haijafahamika kama mtoto Davota ni mlemavu au la na kwamba taarifa za afya ya mtoto huyo zitatolewa baada ya madaktari kumfanyia uchunguzi wa kina
- See more at: http://ubalozini.blogspot.com/2014/07/mtoto-wa-miaka-sita-afichwa-chini-ya.html#sthash.dTmMOY6p.dpuf

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox