Baada ya kuwa kupatikana mabingwa wa mabara mbalimbali sasa hivi ni muda wa kupata bingwa duniani kwa upande wa club. Michuano hii hufanyika kila mwaka huko Japan na kuhusisha club kutoa mabara yote ya dunia.
Mwaka huu michuano hii itahusisha club za Barcelona, TP Mazembe, Club America, River Plate, Auckland City na club ambayo itashida kupata uwakilishi kutoka kwenye club ya J League ambapo michuano ndipo inafanyika.
Kwenye hii michuano inatuhusu watanzania moja kwa moja kwasababu TP Mazembe club yenye watanzania itashiriki kuwakirisha Africa. Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta wanatarajia kujiunga na club zao ili kuendelea kufanya mazoezi kujiandaa na michuano hii.
Michuano hii inatarajiwa kuanza tarehe 10 December mwaka huu kwenye uwanja wa Yokohama huko Japan na hatimaye fainali kufanyika 20 December mwaka huu kwenye uwanja huo huo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni