STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 19 Novemba 2015

SIMBA YAWATEMA WACHEZAJI WAWILI AKIWEPO MZEE WA HIRIZI, KIONGERA NA MCAMEROON NDANI YA NYUMBA






Pape N'Daw na Simon Sserunkuma

Klabu ya Simba imetangaza kuwatema washambuliaji wake wawili, Pape N’daw na Simon Sserunkuma.

N’daw raia wa Senegal amezua midahalo baina ya mashabikiwa Simba baada ya Dylan Kerr kumpigia kura ya ndio kila mara, lakini sasa uongozi wa klabu hiyo ya Msimbazi umesema ndiye aliyempendekeza atemwe.

Ndani ya mechi nane, N’daw hajafunga hata bao moja, ameshindwa kuonyesha uwezo wake na ataendelea kukumbukwa na lile tukio la kukutwa na hirizi wakati Simba ikicheza na Prisons. Ni wazi klabu haijaona mchango wake wala kupata kile walichotarajia kutoka kwake, sasa basi.

Sserunkuma alisajiliwa msimu uliopita akitokea Uganda, lakini naye ameonyesha hakuna lolote. Ameshindwa kufanya kazi aliyoitiwa Msimbazi, hana ushawishi.

Wachezaji hao wa kigeni, walionekana hawana afaida yoyote katika kikosi cha Simba licha ya kupata utetezi wa mara kwa mara kutoka kwa benchi la ufundi likiamini huenda wangeweza kung'ara lakini ikawa kinyume.

Akizungumzia kuachwa kwa wachezaji hao Afisa habari wa msimbazi Simba HAJI MANARA amesema uongozi umeridhia na kuamua kuachana na wachezaji hao baada ya kupokea ripoti ya kocha Mkuu wa klabu hiyo DYRAN KERR kutowahitaji ndani ya kikosi chake kwa hivi sasa.

MANARA amesema pamoja na kuachana na wachezaji hao klabu yao inamipango ya kuongeza wachezaji wengine ndani ya klabu hiyo katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili hasa kumuongeza aliyekuwa mchezaji wao PAUL KIONGERA na wachezaji wengine.

Kwa upande mwingine MANARA amefunguka kuhusu mipango na maendeleo ya uwanja wao uliopo maeneo ya Bunju huku akiwapuuzi wale wanaoibeza klabu hiyo kuhusu maendeleo ya uwanja wa klabu hiyo kushindwa kuujenga kwaajili ya matumizi ya wachezaji wake.

Aidha klabu ya soka ya simba inaendelea na mazoezi yake kwaajili ya mzunguko mwingine wa ligi kuu soka Tanzania bara.
 
Wakati huo huo
Kiungo mshambuliaji Mcameroon Doumbia Ernest ametua nchini akipambana kupata nafasi ya kuziba pengo la Pape N’daw ambaye ametemwa rasmi.



Doumbia tayari yuko jijini Dar es Salaam na anatarajia kuanza mazoezi leo akijifua na Simba jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya majaribio na kama atafuzu, atasajiliwa wakati wa dirisha dogo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox