
Katika taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa Simba, kazi kubwa ya Kamati hiyo itakuwa kuratibu shughuli zote za ujenzi wa Uwanja ikiwa ni pamoja na kutafuta fedha za ujenzi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Mbali na Hans Poppe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Aveva amemteua Salim Muhene, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji kuwa Makamu wa Mwenyekiti.
Katibu ni Issa Batenga wakati Wajumbe wa Kamati hiyo ni Ally Suru, ambaye Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Adam Mgoyi ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Crescentius Magori, Imani Kajula na Jerry Yambi.
Kamati hiyo inatarajiwa kukutana Waandishi wa Habari kuelezea mikakati yao juu ya majukumu waliyopewa.
Chanzo: Binzubery Sports
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni