Uongozi wa klabu ya Liverpool leo April 23 2016 umetangaza kumsimamisha staa wake ambaye alikuwa anahusishwa kutumia dawa za kuongeza nguvu michezoni.
Liverpool imeamua kumsimamisha beki wa kimataifa wa Ufaransa anayeichezea klabu hiyo Mamadou Sakho wakati ambao UEFA wanasubiriwa kukamilisha uchunguzi wao.
Sakho ambaye anachunguzwa na UEFA toka March 17 baada ya mchezo wa Europa league kati ya Man United dhidi ya Liverpool Old Trafford, amesimamishwa na Liverpool baada ya kukaa na uongozi na kujadiliana, lakini Mamadou Sakho atakumbana na adhabu kutoka UEFA baada ya uchunguzi wao kukamilika.
BBC radio 5 inasema kuwa Sakho alipatikana na dawa za kusisimua misuli baada ya mechi ya UEFA kati ya Liverpool dhidi ya Manchester United.
Baada ya kuchukuliwa sample na kufanyiwa vipimo Mamadou Sakho anaaminika kutumia ‘Fat Burner’ kwa ajili ya kusisimua misuli, kitu ambacho hakikubaliki michezoni.
Sakho aliyesajiliwa kwa pauni milioni 18 kutoka Paris St-Germain mwaka 2013 amecheza mechi 34 msimu huu ikiwemo mechi 10 katika ligi ya Yuropa.
Alifunga katika ushindi wa Liverpool wa 4-3 dhidi ya Borussia Dormund mnamo tarehe 14 mwezi Aprili na kufuzu katika nusu fainali ya kombe hilo.
Liverpool ambayo ni ya 7 katika jedwali la ligi ya Uingereza inaialika Newcastle siku ya Jumamosi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni