YANGA
SC imetolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1
na Al Ahly jana usiku Uwanja wa Borg El Arab mjini Alexandria katika
mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora.
Al
Ahly inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya awali
kulazimisha sare ya 1-1 Uwanja wa Dar es Salaam wiki mbili zilizopita.
Aliyewafungisha
virago Yanga jana alikuwa ni Abdallah Said aliyefunga bao la pili dakika
ya sita ya muda wa nyongeza baada ya kukamilika kwa dakika 90 za
kawaida za mchezo akimalizia krosi ya Walid Soliman kutoka upande wa
kushoto.
Al
Ahly walitangulia kupata bao katika mchezo huo kupitia kwa kiungo
Hossam Ghaly aliyeunganisha kwa kichwa kona ya Ahmed Fathi dakika ya 52.
Mshambuliaji
wa kimataifa wa Zimbabwe, Donald Dombo Ngoma akaisawazishia Yanga
dakika ya 57 kwa kichwa akimalizia krosi nzuri ya beki wa kulia Juma
Abdul.
Kwa matokeo hayo, Yanga itamenyana na moja ya timu zilizofuzu Kombe la Shirikisho kuwania nafasi ya kupangwa kwenye makundi.
Kwa
Yanga, hii ni mara ya pili kufikia hatua hiyo baada ya mwaka 2007.
Mwaka huo Yanga ilifungwa 3-0 na Esperance ya Tunisia katika hatua ya 16
Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kutoa sare 0-0 Mwanza.
ZILIZOFUZU NANE BORA LIGI YA MABINGWA;
Enyimba
(Nigeria), Al Ahly (Misri), AS Vita (DRC), Asec Mimosas (Ivory Coast),
Wydad Casablanca (Morocco), ES Setif (Algeria), Zamalek (Misri) na
Zesco United (Zambia).
ZILIZOANGUKIA KOMBE LA SHIRIKISHO;
ES
Sahel (Tunisia), Yanga SC (Tanzania), Mamelodi Sundowns (Afrika
Kusini), Ahly Tripoli (Libya), TP Mazembe (DRC), El Merreikh (Sudan), MO
Bejaia (Algeria) na Stade Malien (Mali).
ZILIZOFUZU KOMBE LA SHIRIKISHO;
Kawkab Marrakech (Morocco),
Mounana (Gabon), Misr Makkassa (Morocco), Medeama (Ghana), FAR Rabat
(Morocco), Esperance (Tunisia), Sagrada Esperanca (Angola) na Stade
Gabesien (Tunisia).
Kikosi
cha Yanga kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua,
Vincent Bossou, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Thabani Kamusoko, Simon Msuva,
Haruna Niyonzima, Amissi Tambwe/Malimi Busungu dk68, Donald Ngoma na
Deus Kaseke/Kevin Yondan dk86.
Al
Ahly; Sherif Ekramy; Ahmed Fathi, Rami Rabia, Ahmed Hegazy, Sabri
Rahil; Hossan Ashour, Hossam Ghaly, Hussein El Sayed, Moaem
Zakaria/Walid Soliman dk64, Ramadan Sobhy na Amr Gamal/ Malick Evouna
dk71.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Jumatano, 20 Aprili 2016
YANGA "OUT" YAFA KIUME MISRI, YACHAPWA 2-1 NA AL AHLY
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni