STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 21 Aprili 2016

BAADA YA KUTOLEWA KWENYE LIGI YA MABINGWA, YANGA SASA YAPEWA WAANGOLA



Sagrada Esperanca na ilianzishwa Desemba 22, mwaka 1976 na Serikali ya Angola, ila kwa sasa inamilikiwa na kampuni ya madini ya Almasi, Endiama, ambao pia ni wadhamini wakuu

Na Prince Akbar, CAIRO
YANGA SC itamenyana na Sagrada Esperanca ya Angola kuwania kuingia kwenye makundi ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika, mechi ya kwanza ikichezwa Dar es Salaam kati ya Mei 6 na 8 na marudiano ugenini kati ya mei 17 na 18.
 
Jina la wapinzani hao wa Yanga linatokana na rais wa kwanza wa Angola, Agostinho Neto, maarufu kwa jina la utani Sagrada Esperanca na ilianzishwa Desemba 22, mwaka 1976 na Serikali ya Angola.
 
Baadaye ikawa inamilikiwa na kampuni ya madini ya Almasi, Diamang (sasa Endiama), ambao wanabakia kuwa wadhamini wakuu.
 
Yanga jana ilitolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1 na Al Ahly Uwanja wa Borg El Arab mjini Alexandria katika mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora.
 
Al Ahly imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya awali kulazimisha sare ya 1-1 Uwanja wa Dar es Salaam wiki mbili zilizopita.
 
Abdallah Said aliifungia Ahly bao la ushindi dakika ya sita ya muda wa nyongeza baada ya kukamilika kwa dakika 90 za kawaida za mchezo akimalizia krosi ya  Walid Soliman kutoka upande wa kushoto.
 
Al Ahly walitangulia kupata bao katika mchezo wa leo kupitia kwa kiungo Hossam Ghaly aliyeunganisha kwa kichwa kona ya Ahmed Fathi dakika ya 52.
 
Mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Donald Dombo Ngoma akaisawazishia Yanga dakika ya 57 kwa kichwa akimalizia krosi nzuri ya beki wa kulia Juma Abdul.
 
Kwa Yanga, hii ni mara ya pili kufikia hatua hiyo baada ya mwaka 2007. Mwaka huo Yanga ilifungwa 3-0 na Esperance ya Tunisia katika hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kutoa sare 0-0 Mwanza.
 
Katika kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho na ilitolewa na El Merreikh ya Sudan, ikitoa sare ya 0-0 Mwanza na kufungwa 2-0 Khartoum.

MECHI ZA MCHUJO WA KUWANIA KUCHEZA HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO 
 
Yanga SC (Tanzania) Vs Sagrada Esperanca (Angola)
MO Bejaia (Algeria) Vs Esperance (Tunisia)
Stade Malien (Mali) Vs FUS Rabat (Morocco)
Etoile Du Sahel (Tunisia) Vs CF Mounana (Gabon)
TP Mazembe (DRC) Vs Stade Gabesien (Tunisia)
Ahli Tripoli (Libya) Vs Misr Makassa (Misri)
El Merreikh (Sudan) Vs Kawkab (Morocco)
Mamelodi Sundowns (Africa Kusini) Vs Medeama (Ghana)
(Mechi za kwanza zitachezwa kati ya Mei 6 na 8 na marudiano kati ya Mei 17 na 18, 2016)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox